Licha ya Samsung kuwa ni kampuni kubwa sana lakini bado kuna kesi mara kwa mara huwa inalikabili kampuni hilo, na cha kushangaza hadi zile za uzembe.
Mahakama imeiamuru Samsung ya huko Australia kulipa dola milioni 14 za kimarekani kama sehemu ya penati baada ya kampuni hiyo kukubali kuwa ilipotosha wateja wake nchini humo kuhusiana baadhi ya viepngele katika simu zake
Kipengele hicho ni uwezo wa kuvumilia kutoingia kwa maji –yaaani katika bwawa la kutengeneza au katika sehemu ya bahari—
Taarifa za kupotosha zilifanyika katika toleo la Samsung S7, S7 Edge A5 (2017) A7 (2017), S8, S8 Plus na Note 8 zikiwa zote ni simu za Samsung Galaxy.
Simu hizi nchini Australia pekee ziliuzika Zaidi ya mara milioni 3.1 ikiwa ni idadi kubwa sana ya mauzo.
Ili kuzitangaza simu hizo kati ya mwaka 2016 na 2018 samsung huko Australia iliandaa matangazo 9 ambayo yalisambazwa katika mitandao ya kijamii lakini baadae yalikua kuzua taharuki.
Taharuki hiyo ni kwamba simu hizi zilikua ni salama na zina uwezo wa kutumika katika mabwawa ya kutengeneza (pool) na hata kwenye maji ya baharini
Matangazo hayo ni haya hapa Matangazo 9 Yaliyopelekea Samsung Kupigwa Penati Huko Australia (Ni link Ya Kuyashusha)
Ningependa kusikia kutoka kwako, naindikie hapo chini katika eneo la comment, je hii unemipokeaje? Je unahisi penati hiyo ni sawa?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.