Kumbuka kwa soko la sasa kampuni ya Samsung ndio imeshika soko la simu janja ambazo zinajikunja. Simu zake za kujikunja zimeenda mbali sana ukilinganisha na makampuni mengine.
Kwa sasa Samsung ina vifaa vingi vinavyotumia teknolojia ya kujikunja, tumeshaona matoleo mengi sana ya simu kutoka katika kampuni hii ambazo zinajikunja.
Simu kubwa katika kampuni ambayo ni ya kujikunja inayosubiria kwa hamu Zaidi ni Samsung Galaxy Z Fold na Galaxy Z Flip, hizi zikiingia sokoni zitaleta chachu kubwa mno.
Ukiachana na hayo, bado Samsung wanataka kuhakikisha kuwa wanawaletea wateja wake simu ya kujikuja (teknolojia ya kujikunja) ambayo ni ya bei rahisi kabisa.
Simu hii ni kutoka katika matoleo na muendelezo wa A maarufu kama A-Series, licha ya hii habari lakini bado taarifa rasmi ya juu ya lini simu hii itatoka haijawekwa wazi.
Not happening that soon tho, 2024-2025. At least that's when Samsung aiming to release… https://t.co/qQbwgAff5Y
— No name (@chunvn8888) June 4, 2022
Kumbuka kwa sasa kuna simu nyingi sana ambazo zinakuja kutoka katika makampuni mbali mbali ambazo ni za ujikunja.
Hili linapelekea hai ya kuwa lazima hapo mbele kuwepo na simu janja ya kujikunja ambayo ni bei rahisi, kwa upande wa Samsung wataanza na toleo katika muendelezo wake wa A (A-Series).
Ni wazi kuwa soko la simu janja za kujikunja linazidi kadri siku zinavyozidi kwenda. Taarifa zilizopo ni kwamba kwa kipindi hichi cha robo ya kwanza ya mwaka 2022 simu janja ya kujikunja zimuza simu milioni 2.22 zaidi.
Hilo likiwa ni ongezeko kubwa sana nab ado, kampuni ya Samsung ikawa bado iko kidedea katika mauzo ya aina hiyo ya simu.
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika uwanja wa comment, Niambie je swala la bei wataweza kukabiliana nalo ili kuhakikisha kuwa inakua ya bei rahisi sana?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.