Kwenye dunia ya leo habari za “Chini kwa chini” ndio zinafanya watu wengi duniani waweze kujua nini cha kutegemea bidhaa fulani itakapotoka lakni ni wazi kwamba vitendo hivyo haviwafurahishi wahusika kama Samsung na wengineo.
Apple, Samsung ni makampuni makubwa ambayo imekuwa ikiwasaka wanaovujisha taarifa zinazohusu bidhaa zao kutokana na kwamba vitendo hivyo vinapunguza ile shauku ya watu kuvutiwa kutaka kufahamu simu hii ya Samsung, iPhone au nyinginr tuu ina vitu gani.
Suala hilo kwa sasa Samsung inaliangalia kwa jicho la karibu kabisa na tayari imeshaanza kuweka misingi madhubuti ambayo inatazamiwa kuleta matokeo chanya. Hatua hizo ni:
Onyo kali
Tayari Samsung wameshaanza kutoa onyo kali kwa wabia wake wote kwenye masuala ya kusambaza bishaa kwa wateja kama njia ya kukabiliana na fununu ambazo zinaonekana kurudisha nyuma makampuni.
Hakimiliki
Mbali na kufanya uchunguzi kwa lengo la kuwasaka wale wanaovujishasifa mbalimbali za bidhaa za Samsung lakini pia kampuni hiyo inatoa nyaraka inayozungumzia masuala ya hakimiliki pamoja na sera za walengwa. Hii inatumika kama njia ya kupunguza uwezekano wa taarifa kuvuja.
Je, suala hili linaweza kuisha/kutokomea kabisa?
Kwa uwazi kabisa suala la fununu kuhusu bidhaa fulani kwenye ulimwengu wa wa sayansi na teknolojia ni ngumu sana kuisha kutokana na kwamba lazima tuu atakuwepo mtu/watu fulani wa kuhamisha mizigo kutoka sehemu moja hadi nyingine ndani kwa ndani. Kwa maana hiyo mtu anaweza akatumia nafasi hiyo kupata tarifa za kutosha na kuzipeleka kwa mwingine.
Kwa jinsi hali ilivyo hivi sasa wanaovujisha taarifa mbalimbali za bidhaa wataakuwa kimya kwa muda kuweza kuruhusu kipindi hili kipite salama bila ya mtu kujikuta matatani.
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.