Samsung ambao walitoa Samsung Galaxy S9 na S9 Plus mwezi Februari 2018 huku ikiwa na Android 8 lakini sasa hatimae sasa watu wanaomiliki simu hizo wameanza kupokea taarifa fupi ya kuweza kuhamia Android Pie.
Kwa hakika ambao wanatumia Sammsung Galaxy S9/S9+ wamesubiri kwa miezi kadhaa tangu kutoka kwa toleo la kenda upande programu endeshi kwa simu za Android.
Kwa taarifa zilizopo wanaotumia simu tajwa huko Ujerumani, Uholanzi. Italia, Uswizi wameweza kupata taarifa fupi kuhusu kuweza kupakua masasisho ya Android 9.
Kama imeanza kwa watumiaji wa simu husika kutoka nchi nyingine basi sio vibaya na sisi wengine tukaanza kuangalia upande wa settings>>about phone>>software update ili kuweza kujua kama Android Pie imesharuhusiwa kuja.
Vyanzo: Android Police, GSMArena, Tech Radar