Dunia ya leo inaendelea kusonga mbele kila kukicha na baada ya teknoloja ya 4G katika suala zima la kufanya mawasiliano na matumizi ya intaneti, 5G ipo mlangoni tayari kupata nafasi yake.
Soko linatarajia kuona kuwa baadhi ya chapa maarufu zilizopo sasa zikiboreshwa kwa kuwekewa teknolojia ya 5G walau katika nusu ya kwanza ya mwaka 2019. Samsung Galaxy S10 ni mojawapo ya toleo maarufu linalotarajiwa kuwekewa mfumo wa 5G wakati itakapotoka.
Hata hivyo, kampuni ya Samsung imethibitisha kwamba toleo lake la kwanza la simu ya mfumo wa 5G haitakuwa Galaxy S10. Kampuni hiyo ya Korea Kusini imepanga kuzindua simu za 5G ifikapo mwezi Machi 2019.