Kampuni ya simu za Samsung Galaxy imeanza kufanyia kazi toleo jipya la Android Oreo 8.0 kwa simu zake na inatarajiwa kuanza kupatikana mwanzoni mwa mwaka 2018.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo iliyotolewa na ofisi za Samsung nchini Uturuki haikuweka wazi tarehe au mwezi gani ndipo simu za Samsung Galaxy zitaanza kupata toleo la Oreo. Hata hivo simu zinazotarajiwa kuwa za kwanza kupata toleo la Oreo ni Samsung Galaxy S8, Samsung Galaxy S8 na Samsung Galaxy Note 8.
Mwaka huu simu nyingi za Samsung Galaxy zilipata toleo la Nougat. Samsung imekuwa ikichelewa kupandisha matoleo mapya ya Android kwa kuwa hufanyia kwanza marekebisho kadhaa ili kuendana na simu zake.
Kwa kawaida simu za Pixel ambazo hutengenezwa na Google hupata mapema zaidi matoleo ya Android kuliko simu nyingine zinazotumia mfumo endeshi wa Android.