Je unaweza kumbuka namba ya mwanao, mpenzi wako au watu wako wa karibu? Tafiti zimefanyika na zimegundua kwa watu wengi ni vigumu sana kukumbuka namba za watoto wao au hata zile za ofisini bila ya kutazama katika simu zao, yaani ‘Contacts’.
Kumbuka kitu hiki hapo awali kilikua ni rahisi sana, mtu aliweza hifadhi namba kichwani kiurahisi tuu. Pengine labda watumiaji wa simu wameongezeka na hata uwezo wa simu umeboresha. Unakumbuka zamani ‘phone book’ mtu alikua anatembea nayo kwenye kitabu/diary spesheli iliyojaa namba za watu?. Lakini hayo yote yamebadilika na teknolojia mpya imetudumaza.
Katika tafiti hii iliyofanyika barani ulaya ilionyesha kuwa zaidi ya nusu ya watu wa ulaya hawakuweza kukumbuka namba za watoto wao au hata zile za ofisini bila kutazamia katika simu. Na pia theluthi ya watu hao, hawana la kufanya ili kuwasiliana na wapenzi wao bila ya kuwa na simu zao.
Lawama zinaweza kwenda kwa hii kitu inaitwa “digital amnesia” (Ule usahaulifu wa kidigitali). Ni ule usahaulifu usio wa msingi ambao unatokana na utegemezi wa teknolojia.
Lawana zinaweza kwenda kwa hii kitu inaitwa “digital amnesia” (Ule usahaulifu wa kidigitali). Ni ule usahaulifu usio wa msingi ambao unatokana na utegemezi wa teknolojia.
Watafiti katika Kaspersky Lab, ambao walifanya utafiti dunia nzima, wamesema uwezo wetu wa kutokumbuka vitu kama hivi (namba za simu) ni kwa sababu tunaachia vifaa vyetu vya kidigitali kama simu kutufanyia yote haya.Lakini hata hivyo nani anataka hifadhi hizi namba za simu wakati simu inaweza fanya hivyo, Sio? Sawa lakini kumbe kuna madhara yake makubwa kuliko tunavyofikiri.
Utafiti ulionyesha kuwa asilimia 51 ya wamarekani na asilimia 40 ya watu wa ulaya kwamba walidai kuwa kupoteza taarifa zao ambazo zimehifadhiwa katika vifaa vyao vya kidigitali kunaweza sababisha madhara kwa mwili na akili.
Hii ni ya kweli kabisa kwani hata kwa wanawake na baadhi ya vijana walioulizwa maswali walisema kuwa simu zao ndio sehemu pekee ambayo wanahifadhi picha, meseji na taarifa zao zingine za umuhimu. Bila ya kuwa na ‘back up’ ya taarifa hizo basi kuna hati hati kubwa ya kuzipoteza au hata pale unapoibiwa kifaa chako taarifa hizo zinapotea kabisa.
No Comment! Be the first one.