Kila leo watu wanachapisha habari ndani ya mtandao wa kijamii wenye watumiaji wengi duniani ambapo inaweza kuwa katika mfumo wa maandishi, picha au hata video na ule ukurasa wa mbele ambayo tunaweza kuyaona hayo yote kwenye Facebook unaitwa “Feed” zamani kikiitwa “News Feed“.
Jumanne ya leo, Feb 15 Facebook kupitia ukurasa wake rasmi wa Twitter imeweka wazi kuwa imebadilisha jina la kipengele chake kinachoonyesha machapisho ya watu mbalimbali wanatummia mtandao huo wa kijamii kutoka kuitwa “News Feed” hadi “Feed“. Sababu ya kufanya hivyo Facebook wanasema ni kuendana na kile ambacho watu wanaona kwenye akaunti zao wakati wanapoperuzi kuweza kufahamu mapya ambayo watu mbalimbali wameweka kwenye mtandao huo wa kijamii.
Starting today, our News Feed will now be known as "Feed." Happy scrolling! pic.twitter.com/T6rjO9qzFc
— Facebook (@facebook) February 15, 2022
Katika miaka ya karibuni Facebook imekumbana na misukosuko mingi iliyoiyumbisha na hata kusababisha watumiaji wake kushuka kwa mara ya kwanza baada ya karibu miongo miwili. Facebook ni kama inajiweka mbali na vitu vingi na kufanya kampuni (Meta) ndio kuwa mstari wa mbele kama mwamvuli wa vyote ambavyo vipo ndani yake (Facebook, Messenger, n.k).
Hadi sasa Facebook inawatumiaji wa kila mwezi zaidi ya 2.89 bilioni wakiperuzi, wakiwasiliana na ndugu/jamaa na marafiki wakati wowote ule. Vilevile, Facebook imekuwa kiungo muhimu cha watu kutangaza biashara zao kupitia kurasa, makundi ambayo yanatazamwa na watu wengi duniani.
Ingawa Facebook inaonekana kupoteza umarufu wake lakini bado inapata watumiaji wengi zaidi kuzidi mitandao mingine ya kijamii. Nini ambacho kinawavutia watu?
Vtanzo: GSMArena, The Verge
No Comment! Be the first one.