Kuna umuhimu mkubwa tuu wa kuzifanya simu janja kupakua masasisho mbalimbali ambayo yanakuwa yamesogezwa karibu kutoka kwenye kampuni husika, kwa mwezi Mei Samsung imeruhusu rununu kadhaa kuweza kwenda Android 11.
Samsung ikiwa moja ya makampuni makubwa yanayofanya vizuri kwenye soko la ushindani na ni wazi kabisa wana wateja lukuki ambao wanatumia rununu mbalimbali za kampuni husika. Hivi karibuni kabisa Samsung wameruhusu Android 11 kwenda kwenye simu hizi: Galaxy A02s, Galaxy A11 na sasa Galaxy A12.
Machache ya kuyakuta kwenye Android 11
Masasisho haya yanakuja sambamba na yale ya kiusalama kwahiyo ni vyema kabisa kuyapakua kwani tunafahamu kuwa Samsung walishasema wamelishughulikia tatizo la vipuri vya Qualcomm kwenye baadhi ya simu zao ingawa hawakuweka wazi rununu husika. Hivyo, kwenye masasisho hayo utakutana na mtiririko wa kumbukumbu za taarifa fupi, urembo urembo vinavipitapita wakati unawasiliana na mtu kwa njia ya ujumbe mfupi wa maandishi pamoja mengineyo lakini bila kusahau muonekano murua wa vitu chini ya One UI 3.1.
Masasisho ya Android 11 kwa simu janja tajwa mpaka muda ambao makala hii inaandikwa yalikuwa yakipatikana nchini Panama tu lakini si vibaya kama utaangalia iwapo yameshafika kwenye nchi uliyopo kwa kuingia Settings>>About Phone>>Software Update.
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.