Wanasayansi kutoka Chuo Kikuu cha Cambridge nchini Uingereza wametengeneza mkono wa roboti wenye uwezo wa kupiga kinanda.
Mkono huo wa bandia, uliotengenezwa kwa kutumia mbinu ya printer 3D, unaweza kucheza nyimbo za muziki kwenye kinanda kwa kusogeza mkono.
Wakifafanua kuwa ni vigumu sana kutengeneza harakati za mkono na vidole kama alivyo binadamu, wataalamu hao wamefanikiwa kuiga mkono wa binadamu ambao unaweza kucheza nyimbo rahisi ikiwemo ya Jingle Bells na baadhi ya nyimbo zingine ilizofundishwa.