Mwaka 2020 umekuwa na mengi lakini kubwa zaidi ni kuhusu virusi vya Corona ambavyo vimeyumbisha uchumi wa Dunia kwa asilimia kubwa tuu; kuhusu kiasi gani cha simu zimefika sokoni simu huko ni huzuni!.
Makampuni yanayotengeneza simu janja na kufanikisha kuzisambaza nchi mbalimbali duniani ndio kitu kinachokuja kuzalisha “Mauzo kwenye robo ya kwanza, pili, tatu”. Sasa kutokana na janja la homa kali ya mapafu inayosababisha na virusi vya COVID-19 makampuni mengi kama si yote yamekumbnana na changamoto ya kufikisha bidhaa zao sokoni.
Hata hivyo, Xiaomi na Realme zimeonekana kupanda kimauzo (kama inavyoonekana pichani) mbali na kwamba kampuni nyingi zimeyumba kimapato.
Wataalamu wa kuchambua wa takwimu za mauzo ya simu wanasema kwenye robo ya mbili mwaka huu bado athari ya janga la virusi vya Corona itaendelea kuonekana kwani kuna makampuni yatakuwa yanapambana kujiweka sawa kibiashara hatimae kuongeza faida.
Kiujumla usafirishaji wa simu janja umeshuka kwa 13% ambapo mara ya mwisho hali hiyo kutokea ilikuwa ni mwaka 2014. Samsung, Huawei na Apple ndio zipo tatu bora. Je, kwenye robo ya pili mambo yatakuaje? Tusubiri kuweza kufahamu na TeknoKona tutakubahabarisha.
Vyanzo: GSMArena, Counterpoint