Katika siku za karibuni WhatsApp imekuwa ikifanyiwa maboresho mbalimbali kitu ambacho inaifanya kuzidi kuvutia halikadhalika kurahisisha utumiaji wake kwenye simu janja na kompyuta.
Matumizi ya jumbe za sauti kwenye WhatsApp imetokea kurahisisha watu kutuma na kupokea kilichotumwa hivyo kuifanya kuwa mbadala wa njia ya mawasiliano kwenye programu tumishi husika ambayo pia ina toleo linatotumika kwenye kompyuta. Utakubaliana na mimi kuwa njia ya kutumia jumbe za sauti ina raha yake ingawa si rafiki kwa ndugu zangu viziwi/wenye usikivu hafifu!
Tangu kuletwa kwa kipengele hicho ndani ya WhatsApp kimekuwa kikiboreshwa kwa namna tofauti lakini haikuwa inawezekana kuweza kusimamisha halafu kuendelea kurekoji/kujirekodi jumbe ya sauti lakini hilo sasa linawezekana! Ndio, katika maboresho ambayo yamefanynika siku si nyingi zilizopita inaonyesha watumiaji wa WhatsApp kwenye kompyuta/simu wanaweza kugandisha na kisha kuendelea kurekodi kitu ambacho anataka kumtumia mtu/kundi husika katika mfumo wa sauti.
Hadi wakati makala hii inaandaliwa maboresho hayo yalikuwa yameshafika kwenye iOS na WhatsApp Beta toleo la kompyuta pekee. Kwa upande wa simu za Android bado haijafika huko ingawa inatazamiwa na wao pia watweza kufurahia maboresho hayo ndani ya siku za usoni.
Je, unazungumziaje mfumo wa jumbe za sauti kwenye WhatsApp kulingana na vitu mbalimbali ambavyo vinaweza kufanyika kwenye programu hiyo tumishi yenye watumiaji wengi zaidi ulimwenguni?
Chanzo: WaBetaInfo
No Comment! Be the first one.