India ni nchi mojawapo lenye watu wengi duniani na makampuni mengi yanaangazia soko kwa maana ya wateja kwa jicho la aina yake jambo ambalo linafanya simu nyingi kutambullishwa huko kwanza.
Kwa kuzingatia simu janja itakayoingia sokoni iwe ni ya kuvutia, iuzike kwa wingi lakini pia bila kusahau wateja wanahitaji rununu ya namna gani Realme 8 5G imejikita katika kuvutia wengi hasa wale ambao uwezo wao hauruhusu kununua simu ghali. Wakati naandaa makala hii nilivutia na uwezo wa betri, kamera, ukubwa wa kioo.
Realme 8 5G ina sifa hizi
Kioo :
- Ukubwa: inchi 6.5
- Ubora: FHD+ (1080*2400px, 90Hz); ung’avu wa hali ya juu sana+umbo mithili ya tone la maji kwenye kamera ya mbele upande wa kushoto
Memori :
- Diski uhifadhi: 64GB/128GB+uwezo wa kuweka memori ya ziada mpaka TB 1
- RAM: 4GB/6GB/GB 8
Kamera :
- Kamera Kuu: Samsung GM1 MP 48, 2, na 2+taa ya kuongeza mwangaza sehemu ambazo kuna mwanga hafifu
- Kamera ya Mbele: MP 16
- Kamera zote zina uwezo wa kuchukua picha za mfuo wowote katika ubora wa 1080px
Betri/Chaji :
- Li-Ion 5000 mAh
- USB-C 2.0, OTG+uwezo wa kuchaji haraka kwa nguvu ya 18W (inakaa na chaji kwa angalau saa 118 kama hutaitumia kwa chochote)
Kipuri mama :
- MediaTek Dimensity 700 SoC
Uzito :
- Gramu 185
Programu Endeshi
- Realme UI 2.0, Android 11
Rangi/Bei :
- Nyeusi na Bluu
- GB 4/64-$191 (zaidi ya Tsh. 439,392), GB 4/128-$204 (zaidi ya Tsh. 470,764) na GB 8/128-$231 (zaidi ya Tsh. 533,554) bei ya India
Kuanzia Mei 18 ndio itaningia sokoni na wenye uwezo wa kuagiza tunaweza kufanya hivyo pia tarehe hiyo ikifika. Je, simu hii imekuvutia? Tunakaribisha maoni yako na kumbuka kutembelea tovuti yetu kila siku.
Vyanzo: GSMArena, Gadgets 360
No Comment! Be the first one.