Moja ya mtandao wa kijamii ambao hauna mambo mengi ni Twitter na pengine wengi kutoupenda/kuutumia mara kwa mara kutokana kutovutia kwa vile ambavyo wanapendezwa navyo. Sasa hivi kuna hii ya kuweza kuamua nani awe na uwezo wa kujibu machapisho yako.
Mwezi Mei mwaka huu Twitter ilipeleka kipengele hicho katika hatua ya majaribio ambapo badhi ya watu walipata uwezo wa kuchagua nani awe na uwezo wa kushiriki kujibu kile ambacho kimechapishwa na mhusika.
Kama usipofanya chochote basi yeyote yule ambae ataona chapisho lako atakuwa na uwezo wa kutoa maoni yake lakini ukiamua kufanya mabadiliko utaweza kuamua iwapo watu uliowataja kwenye chapisho tu ndio waweze kujibu ama wanaokufuata kwenye Twitter waandike yao chini ya kile ambacho utakuwa umekiweka.
Inaweza ikawa ni jambo jema au baya kwa wale wapenzi wa Twitter lakini pia hii inatosha kuwa huzuni kwa baadhi ya watu kwani sasa mhusika anaweza akatenganisha wale ambao wanaandika mazuri na kutoruhusu kabisa anaowafahamu kutopata mrejesho mzuri kutoka kwao.
Utajuaje iwapo umezuiliwa kujibu chapisho la mhusika? Iwapo utaona alama ya Dunia hapo maana yake kila mtu anaweza akajibu, watu walio pamoja inamaanisha ni kwa wale tu wanamfuata mhusika ndio itawahusu lakini pia ukiona ishara ya “Kila mmoja” (@) hapo sasa inawahusu waliotajwa pekee kwenye chapisho husika ndio wanaweza wakasema ya kwao.
Je, wewe umefurahiswa na suala hili la Twitter kukupa uwezo wa kupunguza watu wanaoweza kuandika maoni yao kwenye chapisho lako?
Vyanzo: Gadgets 360, The Indian Express
One Comment
Comments are closed.