Baada ya kampuni ya Google kuwanunua wahandisi wake takribani 2,000 na kupata fedha nyingi, sasa kampuni ya utengezaji wa simu janja za HTC imepata pigo jingine kwa aliyekuwa rais wa kampuni hiyo kuachia ngazi nafasi hiyo ya urais.
Bw. Chialin Chang alijiunga na HTC tangu mwaka 2012 ametangaza kujiuzulu nafasi ya mwenyekiti na mkurugenzi Mtendaji na kuamua kufanya shughuli zake za kibinafsi.
Mpaka sasa HTC haijatangaza ni nani atachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Chialin Chang.
Aidha, HTC imetoa taarifa ya kuthibitisha kujiuzulu kwa Bw. Chialin Chang kutoka nafasi ya Urais kwa kumshukuru kujitolea kwake kwa kampuni hiyo kwa muda wa miaka sita na kumtakia mafanikio katika shughuli zake mpya.