Qualcomm ni kampuni kubwa sana inajihusisha na maswala mengi ya teknolojia ikiwemo kuuza baadhi ya vipuri kwa makampuni makubwa kama vile Apple.
Kwa kuwa teknolojia ya simu inakua kwa kasi sana siku hizi basi Qualcomm na yenyewe imeona isisubiri sana imeona kwamba isisubiri ije na simu janja yake.
Kampuni imeamua kushirikiana na kampuni ya Asus na kwa kuanzia wanadai simu hii itaanza kupatikana katika nchi za China, Ujerumani, Ulaya na Marekani.
Mpaka sasa jina la simu janja hii bado halijawekwa wazi lakini makampuni yote mawili yanadai kuwa itakua ya kimapinduzi zaidi. Vyanzo vingine vinasema itaitwa SNAPDRAGON
Kingine ni kwamba Asus wao kwa kiasi kikubwa sana wamehusika na maswala ya ‘Hardware’ huku Qualcomm wakihusika zaidi na ‘Software’
Sifa Zake Kwa Uchache Ni
Inakuja na Inchi 6.78, 144Hz Samsung OLED panel, Ujazo uhifadhi wa GB 512, RAM ya GB 16GB, senya ya alama za vidole (fingerprint), Uwezo wa 5G.
Inakuja na uwezo wa betri wa 4,000mAh huku ikiwa inakuja na Os ya Android 11.
Kama simu nyingi zinavyokuja siku hizi na simu hii itakuja na kamera tatu kutoka megapixel 64, 12MP mpaka 8MP huku zote zikiwa zina uwezo tofauti katika kupiga picha na kuchukua video.
Kamara ya mbele itakua na MP 24.
Simu inatarajiwa kwa mara ya kwanza kuanza kupatika mwezi agosti mwaka huu. kumbuka jina bado haliko wazi moja kwa moja!
No Comment! Be the first one.