Watu wengi wakifikiria kutengeneza programu tumishi basi wanafikiria watu wanaotumia simu za Android au wakati mwingine toleo la iOS/Android zote zikawa zinapatikana kwa wakti mmoja lakini hii haimaanishi soko hilo la programu tumishi (Google Playstore/App Store) halipewi jicho la karibu na wahusika.
Kabla ya programu tumishi kuweza kupatikana kwa watu kuweza kuishusha kwenye Android/iOS ni lazima ipitiwe na wahusika kisha wakiipitisha au kuikataa aliyeitengeneza anapewa taarifa kuhusiana na ombi lake. Wakati mwingine hata kama programu tumishi inapatikana kwenye soko husika inaweza kuondolewa wakati wowote kutokana na sababu mbalimbali.
Programu tumishi zipatazo arobaini na sita (46) zilizotengenezwa na kampuni moja nchini Uchina zimeondolewa kwenye Google Playstore mara baada ya kubainika kutumia mbinu za uongo kwenye matangazo ambapo iliyokuwa ikionyesha mtu amebofya tangazo fulani lakini kube si kweli ili kuweza kujipatia kipato kwani matangazo ndani ya progamu tumishi ni chanzo cha mapato kwa wengine.
Tujiadhari sisi tunaotengeneza programu tumishi kwani usifikiri kwamba iwapo imekubaliwa (kuwekwa sokoni) basi unaweza ukaanza kufanya mambo yasiyofaa, kuna macho mengi na ikibainika tu na wakajiridhisha kuwa kuna ndivyo sivyo inaendelea programu husika inaondolewa.
Vyanzo: Neowin, BuzzFeed News