Taarifa kuhusu WhatsApp kuboreshwa na kumwezesha mtumiaji kuonyesha hisia zake kwenye jumbe zimekuwa zikielezwa mara kadhaa na sasa kipengele hicho polepole kinaonekana kuletwa kwa walengwa.
Taarifa kuhusu ujio wa kipengele kipya ambacho kinamwezesha mtumiaji wa WhatsApp kuonyesha ishara ya kucheka, kulia huzuni, n.k zimekuwa zinaelezwa na kulingana na kile ambacho WaBetaInfo imeweza kukiona inaonekana mambo yametaradadi hivyo hatupo mbali kuweza kuona kitu hicho kizuri.
WaBetaInfo wameweza kuonyesha kuwa kipengele hicho ingawa bado kipo kwenye hatua ya kujaribiwa na hjuko nyuma kuna baadhi ya watumiaji wa WgatsApp kwenye iOS wameweza kujaribu kukitumia kipengele hicho kipya.
Kwa lugha rahisi tunaposema “Uwezo wa kuonyesha hisia kwenye jumbe” ni ile hali ya mtu anakutumia ujumbe kwenye WhatsApp halafu kwa pembeni tuu chini yake upande wa kulia vinaonekana vitu vilivyo kwenye umbo la duara vikionyesha hali ya huzuni, kucheka, kuchukia, n.k.
Kipengele hicho ni sawa na tuu na vile amabavyo mtu anaweza kufanya kwenye Instagram (upande wa jumbe), Facebook Messenger ambapo mtu anaweza akachagua mchoro wa kitu fulani unaoashiria kupendezwa na kitu, huzunbi, kuchukizwa kulingana na ujumbe alioupokes kutoka kwa aliyeutuma.
Bado haijajulikana ni lini watumiaji wote wa WhatsApp wataweza kutumia kipengele hicho na kwa taarifa zilizopo ni kwamba bado kinatengenewa. Tukusihi tuu uendelee kutufuatilia kwani tutaendelea kukufahamisha yanayojiri kwenye ulimwengu wa teknolojia.
Chanzo: WaBetaInfo
No Comment! Be the first one.