Google Play store ndio soko kubwa kabisa la App mbalimbali duniani kuzidi yote. Hii inatokana na kuwa na App nyingi kuliko masoko mengine.
Muonekano huu unaonekana kuwa utaachiwa kote maana tayari umeshajaribiwa kwa kipindi cha muda mpaka sasa.
Hili limetokea baada ya Google kuaona kuna ulazima wa kuleta maboresho ambayo kwa namna moja au nyingine yatasaidia katika ufanisi na uharaka.
Kwa sasa ukiingia katika ‘https://play.google.com/’ lazima utakutana na muonekano mpya tofauti na ule wa mwanzo.
Ukiingia tuu itakupeleka katika ukurasa wa michezo (games) ambapo katika upande wa juu kabisa utakutana na vipengele vya Games, Apps, Movies, na Kids.
Hapo kwa haraka haraka unaweza ukaingia katika eneo ambalo unalitaka, au ukitaka kuokoa muda zaidi unaweza ukaenda katika eneo la kutafuta (search) na ukaingiza chaguo lako.
Baada ya kutazama picha naona mpaka hapo utakua umeyaona mabadiliko sio?
Ningependa kusikia kutoka kwako niandikie hapo chini katika eneo la comment, Hii umeipokeaje?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.