Makampuni makubwa hayawezi kuacha kutangaza bidhaa zake, lakini pia mara zote hutafuta njia za kujitangaza kitofauti zaidi. #Pepsi wapo njiani kuweka matangazo ya kinywaji chao kimoja juu kwenye anga
Makampuni haya yana tabia ya kutumia pesa nyingi sana katika matangazo japokuwa kwa kiasi kikubwa bidhaa zake zinajulikana.
Sasa basi hebu fikiria pale jua likizama alafu unaona tangazo la kampuni fulani, hii itapendezesha anga sana, mpaka jua lichomoze tena anga itakua imejaa na kivutio/vivutio vya aina yake.
Kampuni ya urusi ambayo inaitwa StartRocket kwa ushirika na kampuni la Pepsi wameonyesha nia katika kuhakikisha wanalifanikisha jambo hili. Hii ni aina nyingine kabisa ya matangazo na inawezekana wakawa ndio wa kwanza kuja na tangazo la aina hii.
Kumbuka matangazo haya yatakuwa yanarushwa na satelaiti maalum huko angani. tayari teknolojia hii iko katika mchakato.
Ijulikane pia kuwa matangazo ya aina hii yataleta mapinduzi makubwa sana katika teknolojia hasa katika swala zima la makampuni mbali mbali ya kutangaza. kampuni halijaongea mambo mengi sana kuhusiana na jambo hili.
Bado kuna wengine wanahisi jambo hili bado haliwezi kuwezekana na kwamba kampuni Ya Pepsi linafanya kiki tuu ili tuu watu waiongelee … tazama tweet hizi.
I fact checked this with a Pepsi rep over email
Me: StartRocket says it's struck a deal with Pepsico Russia such that the first orbital billboard will be an ad for an energy drink… Are you able to confirm whether that's accurate?
Pepsi: Nice to meet you! Yes, that’s true.
— Jon of the Dead (2004) (@Jon_Christian) April 15, 2019
Logo ambayo inaonekana katika picha ni logo ya kampuni ya kufikirika ambayo inaitwa LocaCola