Simu janja mara kwa mara zinatoka mpya kila mwaka tena zenye chapa tofauti tofauti, kampuni kama Apple na Samsung ni moja kati ya miongoni mwa makampuni hayo.
Kwa mwaka 2022 tayari orodha imetolewa ya simu ambazo zimeongoza mauzo katika mwaka huo huku kampuni ya Apple ikiwa kinara.
Apple weneyewe wameingiza simu nyingi katika namba orodha hii yanye simu 10 tuu, huku ikiyapita makampuni mengine yote.
Kwa haraharaka ni kwamba Apple imechukua nafasi nane katika orodha ya simu 10 zilizouza sana mwaka 2022.
Nafasi mbili tuu zilizobakia ni simu zile za matoleo ya Samsung’s Galaxy A13 na A03. Huku iPhone 13 ikiwa ni kinara wa mauzo katika mwaka 2023 kwa maana ikiwa imeuza namba nyingi sana.
Orodha hii imeiweka iPhone 13 kama namba moja maana imeshikilia asilimia 28 ya mauzo yote ya simu hizo lakini ni kwa iPhone peke yake.
Vile vile simu hii ilikua ndio simu inayoongoza kuuzika katika masoko yote yale makubwa kama vile China, US, UK, Germany and France na maeneo mengine mengi.
Kingine ni kwamba simu hiyo ilishika namba moja tangia itokea mwezi wa septemba mwaka 2021 mpaka kufikia mwezi septemba mwaka 2021 ambapo matoleo ya iPhone 14 yalitoka.
Na kwa haraka haraka hii ni mara ya kwanza kabisa kwa matoleo ya Pro Max kuyapita kimauzo matoleo ya Pro katika iPhone na mara nyingi huwa matoleo ya Pro Max yanakuwa yamewekewa sifa ndogo sana na mara nyingi katika kamera na mambo madogo madogo.
Samsung Galaxy A13 imechukua nafasi ya nne katika orodha hii iliyotawaliwa na matoleo ya iPhone huku namba 10 ikishikwa na Samsung Galaxy A03
Chanzo: counterpoint
Nngependa kusikia kutoka kwako, naindikie hapo chini katika eneo la comment, je unadhani kwa mwaka huu ni toleo gani la simu litaibuka kidedea katika eneo la mauzo.
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.