Tukitaka kujua makampuni ambayo yanafanya vizuri kwenye tano bora basi Oppo haiwezi kukosekana kwenye orodha na hivi karibuni wamesheherekea mafanikio waliyoyapata yaliyoambatana na uzinduzi wa bidhaa.
Bidhaa za Oppo si haba zimefika Afrika na kwa hakika hata sehemu nyingine duniani vitu vyao vinauzika. Kampuni hiyo huko Shanghai iliandaa tamasha mahususi kabisa kwa ajili ya kile walichoweza kufanikiwa.
Sababu ilivyowafanya Oppo kufurahia mafanikio kiasi cha kuandaatamasha ni kuweza kuuza bidhaa takribani 100 milioni zote zikiwa na teknolojia ya kuchaji kwa haraka sana.
Ktika tamasha hilo pia Oppo walilitumia kutambulisha kifuko cha kukinga Oppo R17 Pro kutodhurika ikianguka, vipeperushi vidogo vidogo kuhusu NFC na kimemeshi cha ziada ambacho kina 10000mAh inayotoa 5V/10A.
Ni wazi kuwa wana kila sababu ya kujivunia kwa kile ambacho wamekifanikisha. Kimemeshi hicho cha ziada kitauzwa kwa karibu $60|Tsh. 138,000.
Vyanzo: GSMArena, The Verge