Pengine soko la Oppo katika nchi ya ujerumani ndio limefikia tamati kabisa, wanachi wa nchi hiyo wamepatwa na mshangao baada ya kushangazwa ka tovuti ya Oppo—katika nchi hiyo.
Ni makampuni mengi huwa yana utaratibu wa kuwa na tovuti ambayo ni spesheli kwa nchi fulani ili kuaendana na soko hilo, hata kampuni ya Oppo ni vivyo hivyo.
Hivi karibuni tuliandika kuhusiana na kampuni ya Oppo na OnePlus, pengine wanaweza wakaachana kabisa na baadhi ya masoko katika bara la ulaya. Soma zaidi kuhusiana na chapisho hili >>HAPA<<
Japokua fununu hizo makampuni yote mawaili yalizikanusha lakini kwa sasa inankua ni ngumu wateja kuamini kwa upande wa Oppo maana wanaona kabisa kuna viashiria kadhaa vikiwa vinaonyesha kwamba kampuni hiyo haiku sawa kama mwanzo katika nchi hiyo.
Kaishiria ambacho wateja wa ujerumani kimewafanya washtuke ni kwamba tovuti hiyo imepunguza vitu (bidhaa) vingi ambavyo ilikua ikiuza moja kwa moja kupitia katika tovuti hiyo kwa nchini humo.
Pengine unaweza ukashangaa kampuni ya Oppo ikawa ndio imeacha kwa muda au imeacha kabisa kuuza simu katika nchi hiyo.
Kumbuka tovuti hiyo bado inapartikana katika nchi hiyo ila hakuna simu hata moja katika kurasa zake ambayo ipo kama bidhaa ya kununua.
Tovuti hiyo ya Oppo imeacha taangazo tuu ambalo linaonyesha kwamba wao ni washirika katika liga ya mabingwa wa ulaya (UEFA Champions League).
Simu maarufu kabisa za kampuni ya Oppo kama matoleo ya Reno 8 na Find N2 Flip nayo hayapatikani katika mtandao huo
Je unahisi kampuni itajirudi kama zamani au unandhani hii ndio mara yake ya mwisho katika uuzaji wa simu janja nchini ujerumani. Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo kwenye eneo la comment
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.