Kutokana na tafiti zilizofanywa na kampuni kubwa kabisa katika maswala ya utafiti (uchunguzi) wa data mbali mbali na uchambuzi imegundulika kuwa simu janja zimeenea kwa kiwango kikubwa.
Kampuni ya Global Data ni kampuni ya 4,000 kwa ukubwa duniani na katika ripoti yake imesema kuwa mpaka kufikia mwisho wa mwaka 2017 ni kwamba wakenya takribani milioni 20.1 watakua wameshajiunga na matumizi ya simu janja.
likitokea hilo basi bila shaka hii inamaanisha kuwa matumizi ya simu janja ndio yatakuwa yanaongoza ukilinganisha na matumizi ya zile simu za kawaida.
Ongezeko la matumizi kwa mwaka huu ni asilimia 16 ukilinganisha na mwaka uliopita. Hii ukifuatilia vizuri utagundua kuwa hili limetokea kwa sababu kuna ongezeko la simu janja nyingi ambazo zinauzwa kwa bei ya chini kabisa.
Pia Global data imeweka wazi kuwa mpaka kufikia mwaka 2022, takribani asilimia 80 ya waKenya wote watakuwa wanatumia simu hizo.
Hili ni jambo jema kwa wakenya kwani matumizi ya simu janja kwa kushirikiana na intaneti huwa yanasaidia mambo mengi sana hasa hasa katika upande wa kukuza uchumi.
Chanzo: Global Data