Google ambao ndio wamiliki wa Programu-endeshaji (OS) ya Android wametangaza jina la toleo hilo la Android ambalo watu walikuwa wakijua kama Android N
Jina kamili la OS hiyo ni Android Nougat. Jina hili limepatikana baada ya kampuni kutoa tamko katika mkutanao wake uliofanyika mwezi uliopita. Katika mkutano huo kampuni ilipendekeza kuwa watu amabao wanaweza kuipatia jina Android N waweze tuma mapendekezo ya majina hayo kupitia mtandao.
Kama kawaida yao Android huwa wanatoa majina ya OS zao katika peremende za aina mbali mbali duniani au hata majina ya vitu vitamu vitamu vinavyoliwa baada ya kupata chakula. Kutoka toleo la kwanza mpaka sasa majina yote ya OS hizo ni peremende na vitu vitamu vitamu tuu
SOMA PIA: Sababu Za Majina Ya OS Za Android Yanatokana Na Majina Ya Peremende!
Os hii mpya kutoka Google inakuja na vitu vingi sana. Baadhi ya vipengele hivyo ni Skrini inayojigawa katika Apps, maboresho katika eneo la Notification, Emoji mpya na mengine kede kede
Introducing #AndroidNougat. Thank you, world, for all your sweet name ideas! #AndroidNReveal pic.twitter.com/7lIfDBwyBE
— Android (@Android) June 30, 2016
Tangazo hili la Upatikana wa jila la ‘Android Nougat’ lilitangazwa katika mitandao ya kijamii kama vile Snapchat na Twitter