Nokia wametoa simu janja (rununu) kadha wa kadha mwaka 2018 na kwa juhudi hizo wanaendelea kujirudisha kwenye nafasi nzuri ya kiushindani kwani safari hii wamekuja na Nokia X7.
Nikikuuliza ni rununu ipi unayoipenda zaidi kutoka Nokia si ajabu ukanitajia simu janja zaidi ya moja ambazo unavutiwa nazo kwa namna moja au nyingine lakini hapo sio mwisho wa wewe kuvutiwa na bidhaa za Nokia hasa kwa upande wa simu janja. Sasa Nokia X7 ina sifa zifuatazo:-
Kipengele |
Nokia X7 |
Kioo | Kioo kina urefu wa inchi 6.18 Full HD LCD (1080+ pixels) |
Muonekamo | Ina umbo la herufi “V” na inafanana kama Nokia 7.1 Plus |
Kipuri mama | Snapdragon 710 ndio iliyowekwa ikiwa ni toleo la karibuni kabisa |
Kipengele |
Nokia X7 |
Kamera | Nyuma: Kamera mbili-MP 12 na MP 13, kama kawaida zikiwa zimetengenezwa na Zeiss.
Mbele: Ina kamera moja yenye MP 20 |
RAM/Diski uhifadhi |
|
Betri |
|
Kipengele |
Nokia X7 |
Bei |
$245|Tsh. 563,500 (4/64GB), $290|Tsh. 667,000 (6/64GB) na $360|Tsh. 828,000 (6/128GB) |
Rangi |
Nyeusi, Nyekundu, Bluu mpauko na Fedha |
Mengineyo |
|
Kwa taarifa tu simu janja husika bado haijaingia sokoni lakini mtu anaweza akaagiza na mara tu itakapoingia sokoni itatumwa.
Vyanzo: GSMArena, Trusted Review, India Today