Kampuni ambayo inamiliki chapa ya Nokia, HMD Global imekuja na simu tatu, simu hizi sio ngeni (tulishaziona zamani) lakini zinakuja na vipengele vipya kabisa.
Hapa ni kama kumbukumbu sio? Simu hizo tatu ni Nokia 8210 4G ambayo hii inaenda sambamba na Nokia 8210 ya mwaka 1999 kwa muonekano kasoro vipengele tuu.
Simu nyingine ni Nokia 2660 Flip ambayo hii ni ya kufunika na kufunua, simu hii ina vibonyezo vikubwa. Ukifikiria kwa umakini utagundua kuwa hii ni nzuri sana kwa watumiaji wenye umri mkubwa.
Toleo la tatu linatukumbusha kabisa katika matoleo ya XpressMusic. Simu hii inajulikana kama Nokia 5710 XpressAudio.
Simu hii inakuja na maajabu kidogo, kama unavyojua matoleo ya simu hizi (XpressMusic / XpressAudio) zinajikita sana katika maswala ya muziki.
Simu hii inakuja moja kwa moja na spika za masikio (bila nyaya) zikiwa nyuma ya simu hiyo.
Ili kuzifikia spika hizo (zilizopo nyuma) inabidi ushushe sehemu ya mfuniko wa nyuma, eneo hilo ambalo spika hizo zinakaa ni sehemu ya kuchajia spika hizo.
Spika hizo zisizo na nyanya zinaweza kutumika na kifaa kingine chochote kama vile kompyuta, simu nyingine n.k lakini vile vile kinachoshangaza ni kwamba simu hii bado inakuja na tundu la spika.
Ukiachana na simu hizo pia HMD Global inakuja na tabiti inayokwenda kwa jina la T10. Tabiti hii ni toleo dogo la tabiti ya Nokia T20.
Tabiti hii ina kamera ya 8MP kama kamera kuu huku kamera ya mbele ikiwa na uwezo wa 2MP. Betri ni 5250mAh RAM 4GB ujazo uhifadhi wa ndani ni GB64.
Upatikani wa vifaa ni mwishoni mwa mwezi huu katika baadhi ya maeneo kabla hazijaanza kusambaa duniani kote.
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika uwanja wa comment, je hili umelipokeaje na uko tayari kutumia kifaa chochote kati ya hivyo?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.