Hii ni moja katika ushirika mkubwa sana ambao umeshawahi kutokea unaohushisha kampuni ya simu za Nokia, HMD Global na kampuni ya Zeiss
Zeiss inasifika sana katika kutengeneza kamera na hata hapo mwanzo Nokia ilikua haijaweka wazi kwanini iliamua kuichagua kampuni hiyo kuwa kama mshirika wake katika hili.
Vyanzo mbalimbali hata hivyo vinasema ushirika huu ulishaisha tangia mwaka 2021 lakini makampuni hayo mawaili yote hayakuweka wazi.
Unaikumbuka Nokia XR20? Ile ndio ilikua simu ya kwanza ambayo ina teknolojia ya kutoka katika kampuni ya Zeiss.
Vile vile ushirika wa kampuni hizi umeweza kudumu kwa muda mrefu na umekua wenye mafanikio sana, kampuni zote mbili zimenukuliwa zikisema maneneo hayo.
Bado makampuni kama vile Vivo Na Sony wanatumia kamara kutoka katika kampuni ya Zeiss, hii inazidi kuaminisha kuwa Zeiss ni kampuni kubwa sana.
Uzuri wa makampuni haya mawili ni kwamba yalikutana na yakafanya kazi kwa pamoja huku bado yalikua yanawapa nafasi makampuni mengine kuweza kufanya nao kazi
Uzuri wa TeknoKona bwana tuko vizuri kampuni hizi mbili zilipoingia katika ushirika huu tuliakuandikia >>HAPA<< mwaka 2017
Ningependa kusikia kutoka kwako, unadhani Nokia imefanya hivyo sababu inakuja na teknolojia yake katika upande wa kamera au inataka kubadili kampuni? Niandikie hapo chini katika uwanjaa wa comment.
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.