Simu ya Nokia 7.2 ipo njiani kuingia sokoni na inakuja ikiwa na moja ya kamera ya kiwango cha juu katika simu janja kwa sasa.
Kampuni ya HMD Global inayotengeneza simu za Nokia na kumiliki hatimiliki ya kutumia jina hilo imezidi kujikita katika kuhakikisha wanatengeneza simu zenye kiwango cha hali ya juu. Baada ya mafanikio ya simu yao ya Nokia 7.1 sasa toleo jipya la 7.2 lipo njiani.
Mmoja wa wafanyakazi wa juu katika kampuni inayotengeneza vipuri vinavyotumika katika simu ya Nokia 7.2 alitweet kimakosa picha za simu hiyo na hivyo kutoa uhakika juu ya taarifa zinazohusu kamera yake.
Simu hiyo inakuja na kamera tatu zikiwa na sensor za aina tofauti ili kuhakikisha ubora wa picha zake.
Taarifa zingine kuhusu simu hiyo zilizovuja mpaka sasa;
- Inakuja na display/kioo cha HD kwa kiwango cha 1080p
- Prosesa ya Qualcomm Snapdragon 660
- Kamera ya Megapixel 48
- Betri la mAh 3,500
- Kuna matoleo ya RAM ya GB 4 na GB 6, pia kwenye ujazo wa diski kuna GB 64 na la GB 128