Baada ya ukimya wa muda mrefu hatimaye simu ya kwanza ya Nokia ipo mbioni kutoka, hii ni baada ya mkataba baina ya Nokia na Microsoft kuisha.
Mwanzoni mwaka huu kampuni kutoka Finland inayojihusisha na utengenezaji wa simu za Nokia ilitangaza kutengeneza simu janja kadhaa zitakazotumia Android.
Mtandao wa Nokia umetoa taarifa zaidi juu ya Nokia 6 moja ya simu hizo ikiwa ni pamoja na kwamba itaingia dukani mwezi ujao.
Nokia 6 inakuja na kioo cha nchi 5.5 na kikiwa na uwezo wa HD, kamera ya nyuma yenye Megapixel 16 wakati ile ya mbele ina Megapixel 8. Simu hiyo pia inakuja na 3GB RAM wakati memori inakuwa na 32GB ambazo pia unaweza ongeza kwa kudumia memori kadi.
Simu hii inategemewa kuwa madukani mwezi Julai (nchini Marekani) na itakuwa inatumia OS ya Android Nougat ambayo ni OS ya kisasa kutoka Google. Simu hii imetengenezwa kuwa imara kwa kuzungushiwa ganda la aluminium na kuipa ubora zaidi, pia itakuja na katika matoleo mawili la laini moja na la laini mbili.
Simu hii inategemewa kuanza kuuzwa katika Amazon nchini Marekani inakuja katika rangi nyeusi isiyong’aa na fedha. Tayari Nokia wametangaza kwamba wataleta simu nyingine ndogo zaidi ya Nokia 6 lakini hiajajulikana hasa ni lini zitaingia sokoni.