Miaka mingi iliyopita (zaidi ya miongo miwili) simu za kukunja na kufunua zilikuwa maarufu sana lakini pia ghali. Kwa mara nyingine HMD Global wametoa Nokia 2720.
Katika utangulizi wangu nimesema “Kwa mara nyingine tena” kwa sababu moja tu kuwa mwaka 2019 walitoa simu yao ya kwanza katika teknolojia ya kisasa iliyo katika mtindo wa kukunja na kufunua, chini ya miaka miwili kupita tangu itoke ya kwanza HMD Global wametoa Nokia 2720 iliyo katika muundo uleule.
Sifa kuu za Nokia 2720
Kwanza kabisa tufahamu kuwa simu tajwa haipo kwenye kundi la “Simu janja“; ni ille ya kawaida kabisa kwa matumizi ambayo hayahitaji uwezo mkubwa wa kifaa husika. Simu hii ina kamera moja yenye MP 2, RAM-MB 512, diski uhifadhi-4GB, uwezo wa betri-1500mAh na kipuri mama-Snapdragon 205.
VIlevile, Nokia 2720 ina uwezo wa kuingia kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii ambapo mtumiaji anaweza kwenda kupakua programu tumishi kama Google Assistant, Google Maps kutoka sehemu husika ndani ya simu. Simu hii inaendeshwa na programu endeshi iitwayo Kai.
SImu hii inauzwa kwa $79|zaidi ya Tsh. 181,700 bei ya ughaibuni na itaingia sokoni Mei 20. Kama unapenda simu za mtindo huo basi naamini utakuwa umefurahishwa na habari hii hivyo unajipanga ili kuweza kuinunua aidha uiagize au usubiri mpaka ifike nchini mwako.
Vyanzo: GSMArena, The Verge
No Comment! Be the first one.