Matumizi ya vikatuni kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii ni jambo la kawaida sana katika miaka ya hivi karibuni na kwenye Instagram imebuniwa namna ya kufikia emoji bila kuzunguka.
Kama utakuwa ni mtu ambae unatumia Instagram hasa vikatuni (emoji) mabalimbali pale unapoandika kitu kwenye mtandao huo wa kijamii utakuwa umebaini ni kwa namna gani hivi sasa ilivyokuwa rahisi kutumia vitu hivyo.
Sasa hakuna haja ya kufungua sehemu ya kutoa maoni ili kuweza kutumia kikatuni bali vimesogezwa kwenye uso wa mbele (chini kidogo ya pale ambapo maelezo ya kile kilichochapishwa).
Maboresho hayo yanapatikana programu endeshi maarufu; Android na iOS. Suala hilo haimaanishi kuwa vikatuni vingine vimeondolewa, la hasha! Bali zile ambazo zinapendwa ndio zimesogezwa karibu.
Vyanzo: The erge, Engadget
3 Comments
Comments are closed.