Kampuni ya Korea Kusini ya Samsung imeuza simu zake za Familia ya Galaxy A takribani milioni mbili ndani ya siku 40 katika nchi ya India.
Mauzo ya simu hizo yalianza mwezi Machi tarehe 1 na kupata mapato ya $500 milioni ambapo malengo ya kampuni hiyo ni kupata $4 bilioni kwa mwaka kutokana na mauzo ya Simu za galaxy A.
Mapema mwezi huu Samsung ilitangaza kuzindua simu ya Galaxy A20, ikiwa ni simu ya nne katika mfululizo wa simu za Galaxy A. Mwezi Machi Samsung ilizindua Galaxy A10 (Tsh. 280,000), Galaxy A30 (Tsh. 565,000) na Galaxy 50 (Tsh. 758,500).
Kupitia Afisa mkuu wa Masoko na Makamu wa rais wa Samsung India, Bw. Ranjivjit Singh alisema wamepata dola za Marekani 500 milioni baada ya kuuza aina tatu za Galaxy kwa siku 40 tu. Aliongeza kusema kwamba hiyo inaweza kuwa ni rekodi ya mauzo kwa simu hizo nchini India.