Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limeweka hadharani namba za simu zinazotumiwa zaidi na matapeli kwa njia ya mtandao na kuwasihi wananchi kutotuma pesa kwa watu wasiowafahamu.
Namba hizo ziliwekwa wazi na Kamanda wa Polisi kanda maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa mwishoni mwa wiki wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Namba ambazo alizitaja kwamba ndio zimekuwa zikitumika sana ni 0758 713 746, 0764 581 220 na 0744 105 579.
Kamanda Mambosasa aliwasihi wananchi kutotuma pesa kwa watu wasiowafahamu na kwamba mbali na namba hizo matapeli wanaweza kutumia namba zingine.
Aidha, jeshi la polisi kwa kushirikiana na kampuni za mawasiliano zimekuwa zikituma ujumbe kwa wananchi kuwatahadhalisha juu ya utapeli wa mtandaoni.
Moja ya ujumbe kutoka Jeshi la polisi ni huu, “Mwananchi, Usikubali kutapeliwa. Usitume pesa kwa mtu usiyemfahamu. Hakiki ujumbe na simu inayokutaka utume pesa. JESHI LA POLISI LINAZINGATIA USALAMA WA PESA ZAKO“.
Kamwe usikubali tena kuwa mhanga wa utapeli wa mtandaoni/watu ambao wanatumia vibaya uwepo wa teknolojia ingawa daima njia ya mtu muongo ni fupi.
Timu ya uandishi wa Kona ya Teknolojia ingefurahi kupata sapoti yako ili iendelee kukuletea habari na maujanja mbalimbali.
Wezesha bando kwa kutuma kiasi chochote kupitia Selcom, kwenye simu yako bofya *150*50*1# kwenye namba ya malipo weka 60751369 jina litakuja TEKNOKONA.