Kampuni ya kutoa huduma za usafiri wa kukodi nchini Kenya, Uber imeanzisha programu ya kuweka siri namba za simu za madereva wake ikiwa ni mojawapo ya njia za kuwafanya wawe salama.
Uber imeweka programu hiyokutokana kwa muda mrefu madereva wake wamekuwa wakitatizwa na suala la usalama. Madereva watakuwa wakimpigia mteja simu bila namba zao kuonekana. Aidha, maelezo zaidi kuhusu mteja yatakuwa yanajitokeza kwenye programu hiyo.
Tangu mwaka wa 2016 Uber imekuwa ikibuni programu mbalimbali zinazolenga kumfanya mteja na dereva kuwa salama kufuatia matukio mengi ya kiusalama kushuhudiwa kwa madereva wake.