Kuna mamba fulani fulani ambazo ni idadi ndogo sana au asiwepo mtu hata mmoja katika eneo fulani ambae anaweza kutaja namba hiyo ya eneo husika.
Katika nchi nyingi za bara la Afrika (Tanzania ikiwemo) kama mtu akiambiwa aeleze maana/umuhimu wa postcode ni wachache sana watatoa jibu sahihi. Suala hili halina ubishi kabisa na hii inatokana na mawasiliano yanayolandana na postcode kutofanyika mara kwa mara au teknolojia hiyo haipo katika nchi husika.
Postcode ni nini?
Postcode ni namba maalum ambayo inatambulisha kuwa barua fulani inafaa kwenda kata fulani; hii sio namba ya sanduku la posta bali inatoa mwongozo kuwa kutokana na namba hizo basi barua husika inamhusu mtu anayeishi mkoa, kata fulani.
Je, Tanzania ina mfumo wa kutumia Postcode?
Ndio, Tanzania ina mfumo wa kutumia Postcode lakini si wengi wanaofahamu kama nilivyosema kwenye utangulizi wangu kitu ambacho kikanisukuma niweze kukileta kwa wengi kupitia TeknoKona ili wengi waweze kujua namba inayotambulisha mkoa na kata husika.
Orodha ya Mikoa (kwa uchache) nchini Tanzania kulingana na kanda husika.
Dar Es Salaam 11000
Kanda ya Kaskazini
Tanga 21000
Arusha 23000
Kilimanjaro 25000
Manyara 27000
Kanda ya Maziwa Makuu
Geita 30000
Mara 31000
Mwanza 33000
Kagera 35000
Shinyanga 37000
Simiyu 39000
Kanda ya Kati
Dodoma 41000
Singida 43000
Tabora 45000
Kigoma 47000
Unaweza kutembelea tovuti ya TCRA kuweza kuchagua mkoa kuweza kuona namba ya postcode katika kata husika. Pia ukitaka kuona kuona orodha kamili ya mikoa pamoja na postcode zao INGIA HAPA.
Vyanzo: TCRA, mitandao mbalimbali
One Comment
Comments are closed.