Mwanzilishi mwenza wa Twitter Jack Dorsey anajiuzulu kama mtendaji mkuu wa kampuni. Nafasi yake itachukuliwa na afisa mkuu wa sasa wa ufundi, Parag Agrawal. Bw Dorsey, ambaye alianzisha Twitter mwaka 2006, amekuwa akihudumu kama mtendaji mkuu wa Twitter na kampuni ya malipo ya Square.
“Hatimaye ni wakati wa mimi kuondoka” Bw Dorsey aliandika katika barua, akisema kampuni hiyo “iko tayari kuendelea“. Bw Dorsey alisema alikuwa na imani kubwa na mbadala wake. “Ninashukuru sana kwa ustadi wake, moyo, na roho. Ni wakati wake wa kuongoza,” alisema.
Bw Agrawal alijiunga na Twitter mwaka wa 2011, na amekuwa mkuu wa teknolojia wa kampuni hiyo tangu 2017. Bei ya hisa za kampuni ya Twitter ilipanda kidogo huku uvumi wa kuondoka kwake ukiibuka.
Habari za kuondoka kwa Mwanzilishi mwenza wa Twitter Bw Dorsey ziliripotiwa kwa mara ya kwanza na CNBC (Chombo cha habari kilichojikita kwenye habari za kibiashara pamoja na habari kuhusu masoko ya hisa) siku ya Jumatatu.
Katika ujumbe wa tofauti na taarifa rasmi ya shirika, Bw Dorsey alitweet: “Sina uhakika kama kuna mtu yeyote amesikia lakini nilijiuzulu kutoka Twitter“.
“Kuna mazungumzo mengi kuhusu umuhimu wa kampuni ‘kuongozwa na mwanzilishi’. Hatimaye ninaamini kuwa hiyo ni kikwazo kikubwa na hatua moja ya kushindwa” aliandika katika barua pepe iliyoambatanishwa aliyotuma kwa wafanyakazi.
Aliongeza kuwa ataondoka kwenye bodi hiyo baada ya muda wake kukamilika.
Chanzo: BBC News
No Comment! Be the first one.