Matumizi ya betri kwenye simu janja/vifaa vya kidijiti yanachagizwa kwa kiasi kikubwa na kiasi cha mwanga ambao unakuwa umeweka kitu ambacho kinasabisha kuhitaji kimemeshi ili kuchaji.
Makampumi mbalimbali yanakuja na kipengele ambacho kitaruhusu kuwa na muonekano wa giza kitu ambacho tayari tumeshakiona kwenye Youtube na hata kuwa mbioni kuwekwa kwenye WhatsApp.
Kwa mujibu wa utafiti waliofanya Google na kukiri kuwa muonekano wa giza unasaidia kutunza ubora wa betri na kuongea kuwa ingawa mwanga mkali/mdogo kwenye simu unaathiri matumizi ya betri lakini pia rangi ambayo mtu amechagua kuwepo kwenye uso wa juu pia inachangia kumaliza umeme wa betri.
Kwa vifaa vyenye kioo cha AMOLED kitakuwa msaada zaidi kwenye utunzaji wa betri kwenye muonekano wa giza kulinganisha na bidhaa ambazo zina kioo cha LCD.
Bidhaa zenye kioo cha AMOLED zina uwezo wa teknolojia za kung’ara hata wakati wa giza kitu ambacho kinaweza kisisaidie kwenye vioo vya LCD kwa sababu havina uwezo huo.
Kwenye Youtube kipengele cha muonekano wa giza ndio kinaonyesha dhahiri ni kwa kiasi gani kifaa husika kinatumia betri ikiwa na muonekano wa giza au ule wa kawaida ambao wengi ndio tunaoufahamu.
Kiasi cha mwanga, muonekano wa giza, maatumizi ya brtri kulinganisha mwanga ukiwa mpaka mwisho, muonekano wa kawaida (kwenye Youtube) na kiasi gani cha betri kinachotumika.
Inashauriwa sana kutoweka kiasi cha mwanga mpaka mwisho lakini pia kutotumia rangi za mng’ao ili kufanya betri la kifaa gusika kuweza kudumu na umeme.
Vyanzo: GSMArena, The Verge
Timu ya uandishi wa Kona ya Teknolojia ingefurahi kupata sapoti yako ili iendelee kukuletea habari na maujanja mbalimbali.
Wezesha bando kwa kutuma kiasi chochote kupitia Selcom, kwenye simu yako bofya *150*50*1# kwenye namba ya malipo weka 60751369 jina litakuja TEKNOKONA.
Ni Mhariri Msaidizi na mtaalamu wa mambo yanayohusu kompyuta. Pia ni mmoja wa wafuasi wakubwa katika teknolojia; Dunia ya sasa inaendeshwa kwa teknolojia.
Wasiliana nami kupitia |ericmato@teknokona.com|