Muda ambao simu janaja inatumia kuchaji mpaka betri kujaa ni moja ya vipengele muhimu makampuni yanayotengenza bidhaa hizo yanaangalia kwa jiho la karibu na hili linaweza kuwa linachagizwa kutokana na ukuaji wa teknolojia.
SIo kitu cha ajabu kabisa kwa miaka ya karibuni kusikia simu ina teknolojia ya kuchaji haraka mathali kuweza kufikia asilimia 80% ya nguvu kwenye betri ndani ya nusu saa au sehemu ya kuchomekea chaji ni USB-C. Ndio, hii yote inaletwa na ushindani kulingana na dunia ya leo inataka bidhaa za namna gani.
Vimemeshi vya hivi sasa kutoka Samsung ni za kiwango cha 15W lakini inaaminika kampuni ipo mbioni kutoa kimemeshi cha 25W ambacho si tu kwamba kitakuwa na uwezo wa kuchaji haraka lakini pia kimemeshi hicho kitakuwa kwenye mfumo wa USB-Type C. Bidhaa hiyo mpya itakuwa na uwezo wa kufanya kazi vyema kwenye Samsung Galaxy A70, A90, S10 5G.
Kwa haraka haraka naamini iwapo kimemeshi hicho kikawekwa wazi basi mpango wa Samsung ni kuvutia watu waweze kununua simu janjaza kwao ambazo zina uwezo wa kukubali kiasi hicho cha nguvu ya umeme utakaokuwa ukiingia kwenye kifaa husika, sijui wewe una mawazo gani kuhusiana na habari hiyo.
Vyanzo: Gadgets 360, GSMArena