Iwapo unatumia toleo la karibu la WhatsApp utakuwa unafahamu vyema kuwa unaweza kupanga muda ambao kile ulichokituma kwenda kwa mhusika kitoweke baada ya muda gani lakini kwa sasa upo mpango wa kuongeza muda.
Mara kadhaa nimekuwa nikiruhusu kile ambacho nimetuma kwa mtu kupitia WhatsApp kitoweke ama kwa lugha rahisi kisionekane tena kwake baada ya muda fulani ambapo kwa mambo yalivyo hivi sasa kipengele hicho kinamruhusu mtumiaji kuweka muda wa wiki moja.
WhatsApp kwa mujibu wa WaBetaInfo wapo mbioni kufanyia maboresho kipengele hicho kwa kuongeza muda kutoka siku saba hadi miezi mitatu (siku 90) hivyo kutoa uwanja mpana kwa anayepokea ujumbe kuweza kuunakili kabla ya muda wa kufutika kuwadia.
Je, ni toleo gani la WhatsApp lina maboresho hayo?
Mamboresho ya WhatsApp mara zote huanza kuonekana/kutumiwa kwa wale wanaotumia toleo la Beta na kwa hili kama unatumia WhatsApp Beta namba 2.21.9.6 upande wa Android basi fahamu sasisho hilo limekufika.
Kwa sisi wengine inatupasa kusubiri mpaka maboresho hayo yatakaporuhusiwa kupatikana kwa wote ingawa haijulikani ni lini italetwa watumiaji wote wa WhatsApp kwenye Android na iOS.
Usiache kufuatilia TeknoKona kila uchwao kwa habari mbalimbali za teknolojia ndani na nje ya Tanzania kwa lugha adhimu ya Kiswahili.
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
One Comment