Uwepo akaunti za uwongo kwenye mitandao ya kijamii ni suala ambalo linakera na sio zuri kwani watumiaji wake wanaathirika kwa namna moja au nyingine.
Serikali ya Uingereza inapanga kupeleka mswada bungeni ambao utawataka makampuni makubwa inayomiliki Facebook, Instagram na nyinginezo ambazo zinafanya biashara hiyo zimetakuwa kutafuta namna ya kukabiliana na akaunti za uwongo kwenye mitandao ya kijamii. Mpango huu ni sehemu tuu ya mswada wa “Usalama wa Mitandaoni” uliotangazwa mwaka jana ambao umeundwa kusaidia watu kupambana na akaunti zisizojulikana mtandaoni.
Serikali ya Uingereza inasema makampuni haya yanayomiliki mitandao ya kijamii ina wajibu wa kuhakikisha akaunti zisizokuwa za ukweli zinakosa nguvu ya kuwa maarufu kwenye mitandao ya kijamii husika.
Hapa serikali ya Uingereza imeshayauri makampuni haya makubwa ambayo yapo kwenye biashara zinazohusu teknolojia kutumia njia za kuhakiki sura kupitia picha inayowekwa kwenye wasifu (profile), kutumia njia-mbili za uidhishwaji au kitambulisho kitachotambuliwa na serikali.
Katika hatua nyingine, serikali ya Uingereza pia imeshauri kuwepo na mipango itakayolazimisha Facebook, Instagram, Twitter na wengineo kuchuja vitu ambavyo ni halali lakini si vizuri lakini pia kuangalia namna ya kumwezesha mzazi kuweka mpangilio ambayo itazuia mwanae kuona, kupata matokeo ya kile anachojaribu kutafuta kuhusu mada fulani au vitu ambavyo ni si vizuri kuonekana.
Madhara?
Iwapo makampuni haya hayafanya kama ambavyo mamlaka inawataka kuwalinda watu kwenye mitandao ya kijamii basi wanaweza kupigwa faini ya 10% ya mapato yao kitu ambacho kinaweza kuwa mabilioni ya dola kwa makampuni kama Google na Facebook.
Twitter imesema inapitia kile ambacho imeshauriwa kufanya lakini wanasema kuna wakati “Kutojulikana” ni muhimu ili kuweza kusema yale ambayo yanfanywa kinyume na serikali iliyopo madarakani.
Vyanzo: Engadget, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.