Ukiwa unaperuzi kwenye Twitter ukaona akaunti ikiwa na alama ya pata kwa pembeni upande wa kulia hakika mtu huyo atakuwa ana kitu cha ziada ambacho kimemfanya aweze kuwekewa alama ya kipekee ishara ya kwamba ameidhinishwa!.
Kila siku Twitter inaidhisha akaunti za watu lakini kuna taarifa kuwa mtandao huo wa kijamii upo kwenye hatua za mwisho katika kuleta mchakato mpya ambao unahusisha hatua mbalimbali ambazo itakuwa ni LAZIMA kwa yeyote atakayeomba akaunti yake itambulike kwa namna ya kipekee.
Je, mtu yeyote anaweza kuomba akaunti yake ya Twitter iidhinishwe?
Jibu ni ndio lakini lazima iwepo sababu maalum ya kwanini Twitter waiwekee alama ya kipekee mathalani unaweza kuwa mtu maarufu (mwanamuziki, mwanamichezo, n.k), serikali, mwanaharakati na si hivyo tuu bali ni lazima wahusika wajiridhishe kuwa unastahili kupewa kile ulichoomba kulingana na vigezo walivyoviweka.
Alama ya pata inaashiria kuwa akaunti husika imeidhinishwa na ipo kundi maalum.Sio wote wanaoomba akaunti za ziidhinishwe maombi yao yanapita. La hasha! Zipo ambazo zinakataliwa.
Katika mpango huu mpya Twitter inafanyia kazi kile ambacho ilisitisha mwaka 2017 ukihusisha mchakato wa maombi ya akaunti kuidhinishwa ambapo mhusika atatakiwa kujibu maswali kipengele baada ya kipengele kabla ya kuyatuma kwenda kwa wahusika kwa ajili ya kupitia na hatimae kukubali ama kukataa kilicholetwa mbele yao.
Mchakato mpya wa kuidhinisha akaunti ambao Twitter inafanyia kazi.
Kuhusu lini tutaanza kuyaona maboresho hayo mapya (kuidhinisha akaunti) haijulikani lakini taarifa zainasema Twitter wapo kwenye hatua za mwisho kukamilisha suala hilo.
Wezesha bando kwa kutuma kiasi chochote kupitia Selcom, kwenye simu yako bofya *150*50*1# kwenye namba ya malipo weka 60751369 jina litakuja TEKNOKONA.
Ni Mhariri Msaidizi na mtaalamu wa mambo yanayohusu kompyuta. Pia ni mmoja wa wafuasi wakubwa katika teknolojia; Dunia ya sasa inaendeshwa kwa teknolojia.
Wasiliana nami kupitia |ericmato@teknokona.com|
One Comment