Tuzo za zinazojulikana kama IPPAWARDS zimefanyika kwa mwaka 2021 na iphone 5s imeshinda moja kati ya picha bora (iliyopigwa na simu hiyo).
Hii ni ya kushangaza sana kwani iPhone 5s ilizinduliwa mwaka 2013 na mpaka sasa inatimiza miaka nane sasa inawezekana vipi simu hiyo ishinde kama mpigaji picha ya mwaka?
Kumbuka simu nyingi sasa hivi tumeziozea zikitoka mpaka na kamera tatu na nyingine zikiwa zinakuja na kamera nyingi kuliko hizo.
Ukiachana na hayo kwa iPhone tuu kuna mabadiliko mengi, yaani yale ya hardware na hata software kwa iPhone hizi mpya ukilinganisha na iPhone 5s ya mwaka 2013.
Katika tuzo hizi unaweza dhani kuwa kuna matoleo mengi mapya ya simu ambazo zimechukua tuzo. Ni kweli kuna picha 54 ambazo zimechukua tuzo hizi.
Cha kushangaza ni kwamba kati ya hizo 47 zilipigwa na simu za zamani ukiachana na 7 tuu ambazo zilikua zimepigwa na iPhone 12 au iPhone 12 Pro Max.
47 ya picha hizo zimepigwa na iPhone X, iPhone XR, and the iPhone 7, na simu zingine zingine. Pia ukitaka kuona list ya simu ambazo zimechukua ushindi ingia –> HAPA <—
No Comment! Be the first one.