Magwiji wa mitandao ya kijamii kama Facebook, Microsoft, Youtube na Twitter wamekubaliana kuunda kundi la kikazi la kimataifa litakalokuwa likishughulika kuondoa ujumbe au maudhui yoyote yanayoashiria kazi za kigaidi mitandaoni.
Hatua hiyo ya kampuni hizo za mitandao ya kijamii imefanyika kufuatia shinikizo hasa kutoka Marekani na Ulaya kwa kuwataka kuwa na ufumbuzi wa kuondoa ujumbe wowote unaoonekana wenye maudhui ya kigaidi.
Ujerumani wameunda sheria itakayo toa faini ya uero milioni 50 kwa mtandao wowote wa kijamii ambao utashindwa kufuta ujumbe wa kigaidi uliowekwa katika mtandao husika.
Makampuni hayo yameahidi kuanzisha suluhisho la kiteknolojia la pamoja kupiga vita ugaidi mitandaoni.