Rais wa Misri, Abdel Fattah al-Sisi, Agosti 18 amesaini sheria mpya ambayo inawabana watu kutumia mtandao ya kijamii kwa kiwango kikubwa.
Lengo la kupitisha sheria hiyo serikali imesema kwamba hatua hiyo mpya ni katika jitihada za kukabiliana na ugaidi na vurugu za aina yoyote ambazo zimekuwa zikisababishwa na uchochezi kupitia mitandao.
Sheria hiyo ya mtandao ina nguvu ya kuzuia tovuti nchini humo ikiwa zinaonekana kuwa tishio kwa usalama wa taifa hilo au uchumi wake.
Mtu yeyote atakayepatikana na hatia ya kuendesha, au kutembelea, tovuti za aina hiyo anaweza kufungwa au kulipishwa faini na kwa mujibu wa gazeti la Al haram limesema faini ya kosa hilo $10,000 au kifungo cha miaka miwili jela.
Taasisi iliyopo Cairo inayoangazia uhuru wa kufikiri na kujieleza imesema zaidi ya tovuti 500 zimeshafungwa hadi sasa nchini Misri tangu mwaka 2017 hata kabla ya sheria hiyo mpya kuanza kutumika.