Usalama wa vitu vyetu vya kidijitali ni muhimu sana hasa ukizingatia ulimwengu huu buliotawaliwa na teknolojia ambapo bidhaa nyingi ni ghali. Ni kitu kizuri kama inawezekana kutunza Air Tag na AirPods Pro sehemu moja.
Wengi wetu tunafahamu bei ya AirPod Pro; kwa kifupi tuu ni ghali lakini pia ni ndogo kwa umbo kiasi kwamba kuwa rahisi kupotea hivyo kuleta majonzi kwa aliyepotelewa/kuibiwa. Pengine hii inaweza kuwa ndio sababu kuu ya kuwafanya Apple kutengeneza kifaa kidogo ambacho kinaweza kufuatilia bidhaa fulani iwapo Air Tag ipo karibu na bidhaa husika ambayo mtu asingependa kuipoteza.
Halikadhalika, kwenye AirPods Pro kuna ubunifu mpya umefanyika ambapo mfuko huo unaweza kutunza vitu hivyo viwili kwa pamoja na usalama. Mfuko huo uitwao Tag Armor Duo unauzwa $35|zaidi ya Tsh. 80,500 bei ya ughaibuni inaweza kukupa hafueni ya kujua zilipo AirPods Pro ambapo zinauzwa $249|zaidi ya Tsh. 572,700 kutoka kwa Apple wenyewe.
Hii ni bidhaa ambayo kiukweli inavutia na hata kushawishi kuinunua hasa kwa sisi ambao tunapenda kuburudika kwa muziki mzuri kupitia simu janja zetu. Karibu ewe msomaji wetu kutupa maoni yako kuhusiana na bidhaa hii.
Vyanzo: Engadget, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.