Meta inamiliki mitandao ya kijamii ya WhatsApp, Facebook Na Instagram. Pengine hili sio la kushangaza sana maana tokea mwanza tunajua kama mitandao hii mitatu inaingiliana kwa namna moja au nyingine.
Hata whatsApp wakati unatumia ‘status’ kuna kipengele cha kutuma ‘status’ hiyo moja kwa moja katika mtandao wa Facebook kwa sasa Meta inadai ni zamu ya Instagram na Facebook kwenye upande wa Reels
Hii inakuaja baada ya makampuni ya Facebook na Instagram kuwa na mkakati wa kusaidia wazalishaji wa maudhui kufikia watu wengi Zaidi kwa kuwaruhusu ku’post maudhui sawa katika mitandao hiyo yote miwili kwa urahisi.
Vyanzi mbalimbali vinaeleza kuwa kampuni hizo zinazomilikiwa na Meta zinapitia yote hayo huku kampuni ikiwa na dhima ya kuleta ushindani na mtandao wa TikTok.
Hata muda mrefu haujapita, unakumbuka wakati mtandao wa Instagram ulitoa kauli kuwa inajikita sana katika video japo hili liliwakera wengi.
Watu wanachoamini ni kwamba mtandao huu umejulikana sana kupitia swala zima la picha, kinachooekana ni kwamba mtandao huu unafuata nyayo za TikTok na Snapchat—pengine kuna ukweli sio?
Meta inasema kuwa kama huduma hii hujaipata katika mitandao yao kwa sasa huna budi kusubiri kwani huduma hiyo inaachiwa kwa wote –kingine cha kuhakikisha ni kuwa na sasisho jipya kabisa la mitandao hiyo.
Ningependa kusikia kutoka kwako, naindikie hapo chini katika eneo la comment, je wewe ni mtumiaji mzuri wa huduma hizi? Na uko tayari kwa Real moja kupanda moja kwa moja katika mitandao hii miwili?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.