Meta ni kampuni ambayo inamilikia mitandao maarufu sana ya kijamii ya WhatsApp, Facebook na Instagram. Kwa sasa kampuni iko na mpango wa kuongeza vipengele vya kulipia katika mitandao hiyo.
Cha msingi kujua hapa ni kwamba kama kipengele au vipengele hivyo vikitolewa basi vitakua vikitumika na hao ambao wataamua kulipa tuu katika mitandao ya kijamii ya Meta
Kumbuka kwa sasa kuna vipengele vingi sana katika mitandao ya Instagram na Facebook ambavyo ni vya kulipia na hasahasa ni matangazo lakini mtandao wa WhatsApp bado uko nyuma kidogo sio?
Kingine ni kwamba kampuni inafanya hivi ili kujihakikishia kuwa inazidi kupata mapato mengi kutoka katika vyanzo mbalimbali ukiachana na kutegemea na vile vya mwanzo tuu.
Mpaka sasa lakini ni wazi kwamba haijulikani ni kipengele gani ambacho kampuni itakuja nacho katika kuhakikisha kuwa mitandao hiyo yote mitatu inajiongezea mapato.
Cha kutilia akilini ni kwamba kampuni ya Meta ndio kampuni kubwa ambayo inamiliki mitandao mitatu ya kijamii ambayo ni mikubwa sana kwa sasa hivyo haiwezi kushindwa jambo kwa urahisi.
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika uwanja wa comment, je hili umelipokeaje? Je unadhani ni sasa kwa kampuni kuzidi kuongeza vipengele vya kulipia?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.