Nianze na swali, ni kwa kiasi gani kipindi hiki unawasiliana na ndugu, jamaa na marafiki? Si ajabu ukafurahishwa na hili kwa kitendo cha Facebook kuweka Messenger rooms ndani ya WhatsApp.
Kwa kipindi hiki ambacho si jambo zuri sana kukutana na watu ana kwa ana bila ya kuwa na tahadahri ya kiafya basi ni vyema tukafikiria njia mbadala za kuweza kuonana na watu kwa njia ya kidijiti.
Mwezi jana Facebook walitambullisha “Messenger Rooms” na kukiruhusu kufanya kazi siku chache tuu zilizopita ndani ya Facebook messenger lakini sasa kipengele hicho kimesogezwa kwenye WhatsApp beta toleo 2.20.163 kwenye Android pekee.
Je, Messenger rooms ni nini?
Hiki ni kipengele ambacho kinamuwezesha mtu anayetumia Faccebook Messenger kuweza kuwasiliana na jamaa zake kwa njia ya picha mnato (jongefu). Hapo mtumiaji ataweza kuwasiliana na marafiki zake hadi watu hamsini (50) kwa wakati mmoja.
Je, inapatikana kwa watumiaji wote wa WhatsApp?
Ukiacha kwamba kwa sasa inapatikana kwa wanaotumia simu janja za Android tu lakini kipenge hicho pia kimeruhusiwa kwenye baadhi ya watu na nchi pia lakini tutarajie kukiona katika siku za usoni kikipatikana kwa watu wengi zaidi wakiwemo wale wanaotumia rununu zenye iOS.
Inawezekana inakuaje Facebook ina uhuru wa kupeleka maboresho kwenye WhatsApp? Hii ni kwa sababu Februari 19 2014 alinunua WhatsApp na hivyo kuwa chini yake.
Vyanzo: GGSMArena, WABetaInfo