Teknolojia ya leo wala haihitaji kwenda mbali ili kuweza kupata mchezo fulani bali kwa kutumia kifaa chako cha kiganjani na ukaweza kuburudika/kushinda katika hali nzuri kabisa.
Nikiwa kama mtu mmojawapo ambae napendelea kutumia michezo (magemu) kuiburudisha akili yangu baada ya kazi ngumu huwa sichezi mbali na vile ambavyo vinaniburudisha na katika pitapita zangu nikakutana na hiki ambacho kitatufaa wengi kutokana na kuwa na wateja wengi.
Halotel Tanzania wameweza kufikiria kitu ambacho kingewza kuonekana kutokuwa na mantiki kwa idadi kubwa ya watu lakini pengine sasa itapendeza kutokana na kile ambacho atazawadiwa akibahatika kushinda.